Diamond Platnamz ameamua kutoa yake ya moyoni baada ya kumshida
kuyavumilia.Kutokana na maelezo yake aliyoyaandika kupitia ukurasa wake
wa Instagram, inaoneka amekerwa na tabia ya wasanii wenzake kumsema
vibaya na kutengenezea ugomvi wa kilazima pasipokuwa na sababu, wakati
yeye anahangaika na mziki wake kivyake...
"kiukweli, nasikitishwa sana jins baadhi ya wasanii kutwa wanavyolazimisha kunitengenezea ugomvi wa kilazima pasipo kuwa na sababu, mara wengine
wakizusha eti Nimewatusi kwenye Media, Mara sjui Nimepost kuwakashif, yaani
ilimradi tu....kwanini Wanamuziki wa Tanzania Tunashindwa kubadilika... mbona mi nahangaika na muziki wangu kimpango wangu... Mnasema nyie ndio mnaojua kuimba
mie sijui "sinatatizo"... Mnasema nyie ndio wenye sauti nzuri yangu mbaya "Sina tatizo"... sasa mbona tena bado mnanifatilia na kutokujua kwangu... Nafkiri ni vyema
mkaanza kutumia ujuzi wenu kukuza sanaa ya nchi yetu na kuleta heshima na maendeleo nchini, kuliko kupika majungu..... Watu wanataka kazi!"
0 comments:
Post a Comment