Pages

Search This Blog

Powered by Blogger.

Saturday, January 19, 2013

Watekaji nyara na mateka wauawa Algeria

 18 Januari, 2013 
Kiwanda cha gesi
Harakati za wanajeshi kujaribu kuwaokoa raia wa kigeni waliozuiliwa mateka na wapiganaji katika kiwanda kimoja cha kutengeneza Gesi nchini Algeria zimesababisha vifo vya wapiganaji kadhaa huku mateka wao wakiwa hawajulikani waliko.
Idhaa ya Serikali imesema kikosi maalum cha wanajeshi bado kimezingira sehemu ya kiwanda hicho ambako wapiganaji hao bado wanawazuilia mateka kadhaa.
Kulingana na Maafisa wa Serikali, mateka na wapiganaji waliuawa kwenye makabiliano ya awali, huku taarifa za wapiganaji hao ambazo hazijathibitishwa zikidokeza kuwa raia 35 wa kigeni waliokuwa wamezuiliwa mateka na watekaji nyara 15 waliuawa.
Taarifa za vyombo vya habari zinasema kuwa wanamagmbo wanne wameuawa. Walikuwa wanadai kuwazuilia mateka 41.
Baadhi ya mateka hao waliachiliwa lakini idadi ya walionusurika ilithibitishwa na maafisa wa serikali ya Uingereza ikisema kuwa inajiandaa kwa taarifa za majeruhi wengi wa Uingereza.
Wapiganaji hao wenye uhusianao na kundi la Al-Qaeda, walivamia kituo cha Amenas siku ya Jumatano.
Wakati wa harakati zilizofanywa siku ya Alhamisi, waalgeria wengi pamoja na mateka wanne wa kigeni, wawili kutoka Scotland, mmoja mfaransa na mwingine mkenya waliachiliwa.
Serikali ya Scotland, ilithibitisha kuachiliwa kwa mmoja wa raia wake. Mateka watano wa Marekani pia walinusurika na kuweza kuondoka nchini humo mara moja kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Marekani.
Japan nayo ilisema kuwa raia wake watatu waliachiliwa wakati wa harakati za jeshi lakini wengine 14 hawajulikani waliko.
Mapema wanamgambo walisema kuwa mateka 34 na wapiganaji 14 waliuawa huku saba wakinusurika.
Duru zinaarifu kuwa jeshi la Algeria halijaweza kudhibiti eneo hilo lote na kwamba msako ungali unaendelea.
Wanamgambo walisema kuwa walifanya shambulizi hilo kama kulipiza kisasi hatua ya Ufaransa kuingilia hali ya Mali.

0 comments:

Post a Comment